15.1 Tusome kwanza maandiko katika Mwanzo 15:1-21
Back to: KOZI 101: KITABU CHA MWANZO
MWANZO 15:1-21
- Baada ya mambo hayo neno la Bwana likamjia Abramu katika njozi, likinena, Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana.
- Abramu akasema, Ee Bwana MUNGU, utanipa nini, nami naenda zangu hali sina mtoto, na atakayeimiliki nyumba yangu ni huyu Eliezeri, Mdameski?
- Abramu akasema, Tazama, hukunipa uzao, na mtu aliyezaliwa nyumbani mwangu ndiye mrithi wangu.
- Nalo neno la Bwana likamjia likinena, Huyu hatakurithi, bali atakayetoka katika viuno vyako ndiye atakayekurithi.
- Akamleta nje, akasema, Tazama sasa mbinguni, kazihesabu nyota, kama ukiweza kuzihesabu. Akamwambia, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.
- Akamwamini Bwana, naye akamhesabia jambo hili kuwa haki.
- Kisha akamwambia, Mimi ni Bwana, niliyekuleta kutoka Uru wa Wakaldayo nikupe nchi hii ili uirithi.
- Akasema, Ee Bwana MUNGU, nipateje kujua ya kwamba nitairithi?
- Akamwambia, Unipatie ndama wa miaka mitatu, na mbuzi mke wa miaka mitatu, na kondoo mume wa miaka mitatu, na hua, na mwana njiwa.
- Akampatia hao wote, akawapasua vipande viwili, akaweka kila kipande kuelekea mwenzake, ila ndege hakuwapasua.
- Hata tai walipotua juu ya mizoga Abramu akawafukuza.
- Na jua lilipokuwa likichwa usingizi mzito ulimshika Abramu, hofu ya giza kuu ikamwangukia.
- Bwana akamwambia Abramu, Ujue hakika ya kwamba uzao wako utakuwa mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia watu wale, nao watateswa muda wa miaka mia nne.
- Hata na taifa lile, watakaowatumikia, nitawahukumu; baadaye watatoka na mali mengi.
- Lakini wewe utakwenda kwa baba zako kwa amani, utazikwa katika uzee mwema.
- Na kizazi cha nne kitarudi hapa, maana haujatimia uovu wa Waamori bado.
- Ikawa, jua lilipokuchwa likawa giza, tazama, tanuru ya moshi na mwenge unaowaka ulipita kati ya vile vipande vya nyama.
- Siku ile Bwana akafanya agano na Abramu, akasema, Uzao wako nimewapa nchi hii, kutoka mto wa Misri mpaka huo mto mkubwa, mto Frati,
- Mkeni, na Mkenizi, na Mkadmoni,
- na Mhiti, na Mperizi, na Mrefai,
- na Mwamori, na Mkanaani, na Mgirgashi, na Myebusi.
YESU.PROSHABO.COM
0